
Dar es Salaam. Unakumbuka yule shabiki wa Yanga maarufu kwa jina la Steve Yanga au Shabiki wa kulialia?, SasaNni kwamba ameibuka na kihoja kipya baada ya kutangaza kutoishabikia tena timu hiyo na kusema yuko njiani kuhamia Simba au Azam FC.
Akizungumza na gazeti hili jana, Steve ambaye
aliwahi kuzawadiwa pikipiki na mMwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji
kutokana na kuwa na mahaba mazito na klabu hiyo, alisema ameamua
kuikacha timu hiyo baada ya kukwaruzana na baadhi ya viongozi wa klabu
hiyo.


“Ukweli ni kwamba, Yanga imenifanya niwe mtu
maarufu ndani na nje ya nchi, lakini nimeamua kuacha kuishabikia tena
baada ya kutukanana na viongozi.
“Kuna siku nilimpigia simu na kiongozi mmoja wa
zamani wa Yanga wa zamani (jina tunalihifadhianamtaja), alinitukana
kisha akakata simu. H, hili tukio lilinikwaza sana ndiyo maana
nimechukua uamuzi huo,” alisema Steve.
”Kwa sasa natafakari kwanza, lakini nipo njiani kuhamia timu moja wapo kati ya Simba au Azam FC.,”.
Wakati Steve akichukua uamuzi huo, shabiki
mwingine maarufu wa klabu hiyo Ali Mohamed ‘Ali Tumbo’ alisema kitendo
kilichofanywa mwenzake ni kujidhalilisha.
“Hata mimi napenda fedha, lakini siyo kwa staili iliyofanywa na huyu Steve. H, huku ni kuendekeza njaa kulikopitiliza... ,yaanin amejidhalilisha,,” alisema.
“Hata mimi napenda fedha, lakini siyo kwa staili iliyofanywa na huyu Steve. H, huku ni kuendekeza njaa kulikopitiliza... ,yaanin amejidhalilisha,,” alisema.
No comments:
Post a Comment